AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Manowari ya USS John MacCain ilikuwa mashariki mwa Singapore ikijiandaa kutia nanga bandarini wakati iligongana na meli iliyokuwa ikipeperusha bendera ya Liberia.
Shughuli kubwa ya kuwatafuta na kuwaokoa wanajeshi inaendelea
Ndicho kisa cha pili kikubwa kinachoikumba meli ya jeshi la wanamaji wa Marekani miezi ya hivi karibuni.
Ripoti zinasema kuwa manowari hiyo ilikumbwa na uharibifu upande wake mmoja, lakini jeshi la Marekani lilsema kwa inaelea peke yake kwenda bandari ya Singapore.
Map shows the location of Singapore and the Strait of Malacca
Helikopta za jeshi la Marekani na jeshi la Singapore pamoja na walinzi wa pwani, wanafanya shughuli za uokoaji. Malaysia nayo imejiunga katika shughuli hiyo.
Kura taarifa kidogo kuhusu hali ya meli ya mafuta ya Alnic MC na wahudumu wake.
Meli hiyo ya mafuta inaripotiwa kuwa na uzito mara tatu wa manowari ya jeshi ya USS John McCain, na taarifa zinasema kuwa haikuwa imebeba mafuta wakati ya ajali hiyo.
Seneta John McCain ambaye jina lake limepewa manowari hiyo, aliandika kwenye mtandao wa twitter kuwa yeye na mke wake wanawaombea mabaharia hao.
Mwezi Juni mabaharia saba wa Marekani waliuawa wakati manowari ya USS Fitzgerald iligongana na meli ya mizigo kwenye bahari ya Japan karibu na bandari ya Yokosuka.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK