Mimi Nipo Sexy Sana na Nina Mvuto Sidanganyiki na Vichips Mayai – Lulu Diva

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msanii wa Bongo Flava, Lulu Diva amejimwagia sifa jinsi anavyoamini kuwa yeye ni mzuri.

Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha Uhondo cha E Fm kuwa alitambua kuwa yeye ni mzuri kutokana na sifa alizokuwa akipewa na mama yake mzazi kitu ambacho  kilimfanya kutolaghaika na watu waliokuwa wakimsifia.

“Mimi ni msichana ambaye nipo sex ambaye nina mvuto, mama yangu alikuwa akiniambia Lulu mwanangu mashallah, yaani hapa sidhani kama kuna mtu nitamwambia idadi ya ng’ombe ninazozitaka halafu akapindua,” amesema na kuongeza.

“Na mimi mwenyewe nikawa najiona ndio maana hata sikuweza kurubunika, yaani ile mtu kuniambia wewe mzuri akanidanganya kwa vichipsi mayai, mwenyewe nilishajijua ni mzuri,” amesema Lulu Diva.

Hitmaker huyo wa Usimwache kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake inayokwenda kwa jina la Utamu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. LULU DIVA. MIMI MBONA SIKUELEWI...!!! SASA BIASHARA IMEKUWA MITANDAONI. AU UMEKOSA SOKA..!!!?
    KWANI NANI KASEMA WEWE MBAYA?
    AU NDIYO VILE... MANAKE MAJI YAKIGUSA NYAYA LIVE NI HATARI. TULIA DADA.
    ILE POSA ULISHAJIBU..!!! SEMA NI NG'OMBE KICHAA MMOJA NA NDAMA MOJA JUMLA ZINAKUWA TATU. UKIJUMLISHA PAMOJA NA KALE KAKUKU KAMA RODA ANAKAUZA PIA. TUNANGOJA MAJIBU.

    ReplyDelete

Top Post Ad