AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Spika Ndugai amebainisha hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa makabidhiano ya ripoti ya kamati ya uchunguzi wa biashara ya madini ya Tanzanite na Almasi uliofanywa na kamati maalum mbili.
"Kumpata Rais aliyejitoa kusimamia rasimali za nchi si jambo rahisi wala jepesi. Mwalimu alijaribu kufanya hivyo awamu ya kwanza pakawa na tabu mtindo mmoja lakini watanzania walishikana naye kwa magumu yote yaliyokuwepo hadi mwisho kwa hiyo sasa lazima tushikamane na Rais wetu hata kama tunapo kwenda tutakuwa na magumu yeyote yale kwa maana kwamba lazima rasimali za nchi ziwafaidishe watanzania kwa namna moja ama nyingine, hatusemi asilimia 100 iwe yetu hatuwezi kwa sababu tunahitaji teknolojia, fedha na mambo mengine kutoka wa wabia wenye nia njema ili nasi tupate", amesema Ndugai.
Pamoja na hayo, Mhe. Ndugai ameendelea kwa kusema "ndugu zangu watanzania tunapaswa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kumpata Rais Magufuli, sisemi haya kwa sababu yupo mbele yangu, nyinyi wenzangu mnafahamu nchi zetu za Afrika hizi historia zetu za Afrika na jinsi tulivyokuwa tumeneemeshwa na Mwenyezi Mungu lakini wajanja wachache wanachukua mali za
Afrika na kuiacha haina lolote tangu wakati wa mkoloni na baada ya mkoloni", amesisitiza Ndugai.
Kwa upande mwingine, Mhe. Ndugai amewasisitizia wabunge kuwa na umoja katika mambo ambayo yanawaunganisha ambapo moja wapo ni kuhusu rasimali za taifa huku akipiga dongo kwa kusema wanaopaswa kukosa uzalendo ni Simba na Yanga kwa sababu wao wanaimba kabisa uzalendo umewashinda pindi wawapo uwanjani.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK