AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Bulembo aliwahi kusema kuwa hatogombea tena lakini baadaye aliamua kuchukua fomu. Hata hivyo Bulembo amesema aliamua kuchukua fomu ya kugombea baada ya kupata shinikizo kutoka kwa makatibu wakuu na wazee wa jumuiya hiyo.
"Sasa leo(Jumanne) nimewaita kuwaeleza sitagombea tena licha ya kuchukua fomu, naamini wagombea 48 waliopatikana, kuna mmoja atatufaa kuongoza jumuiya hii, leo ninapeleka barua kwa katibu mkuu wa chama (Abdulrahiman Kinana) ya kumweleza dhamira yangu hii,” amesema Bulembo leo Jumanne alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa.
Bulembo amesema uchaguzi katika ngazi ya Taifa utafanyika kuanzia Novemba 20 hadi 23, wagombea wote wapo lakini yeyote aliyeanza kampeni mapema huyo ameshajikata," amesema.
Kuhusu hoja ya kuchukua fomu amesema haikuwa dhambi kwa kuwa kanuni za chama zinaruhusu na upo uwezekano wa kuwa na nafasi mbili za uongozi.
"Kumekuwa na upotoshaji kwamba, ukiwa mbunge au waziri hauwezi kugombea nafasi nyingine, sasa hapa nina kitabu cha kanuni za mwaka 2005, 2010, 2012 na 2017 zinasema kiongozi au mbunge, waziri anaweza kugombea ila kamati kuu ya chama itaamua inavyofaa, kama bado anahitajika atapitishwa lakini mie sitagombea tena,” amesema.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
You have done well toka driver taxi Musoma na kufika kuwa Mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi Hongera
ReplyDelete