Jenerali Mabeyo Awatahadhalisha Wanajeshi Matumizi ya Mitandao ya Kijamii

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jenerali Mabeyo Awatahadhalisha Wanajeshi Matumizi ya Mitandao ya Kijamii
Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo ameagiza wanajeshi kuacha kujihusisha na matumizi mabaya mitandao ya kijamii kwani kufanya hivyo ni kinyume na taratibu za jeshi.

Jenerali Mabeyo amesema hayo leo Jumamosi katika hafla ya kutunuku nishani  ya  Luteni Usu kwa maofisa 422 wa jeshi iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Amesema jukumu la wanajeshi ni ulinzi wa Taifa hivyo kujiingiza katika mambo yasiyofaa ni ukiukwaji wa taratibu za jeshi hilo.

Mabeyo amewataka wanajeshi kuepuka kuliingiza jeshi kwenye siasa na badala yake wanatakiwa kuwa na uzalendo kwa Taifa lao.

“Niwasihi msimame kwenye kiapo mlichoapa leo. Wapo baadhi ya askari husahau kwa haraka na kukiuka kiapo, msifike huko. Matamshi uliyoyatoa leo yanaelekeza wajibu wako, utii, kuilinda katiba, kumtii Rais na kumtumikia.”
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad