Lulu Afunguka Kuhusu Kufunga Ndoa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Lulu Afunguka Kuhusu Kufunga Ndoa
STAA wa sinema za Kibongo ambaye pia alikuwa msanii wa kwanza kuigiza akiwa na umri mdogo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, kwa mara ya kwanza amefunguka kila kitu chake hadharani ambacho wapenzi wake wengi wamekuwa wakijiuliza bila majibu. Lulu amesema kuwa kujiamini ndiko kumemfikisha hapo alipo, ungana nami katika makala haya;
Swali: Watu wengi wamekuwa wakijiuliza unapata jeuri ya kujiremba na kuvaa nguo nzuri kila siku au ndiyo mambo ya mtarajiwa?
Lulu: Unajua siku hizi watu wame-kariri sana kuwa kila mtu akipendeza ni mwanaume, kwa hali ya sasa mwanaume gani anaweza kufanya hivyo kwa mwanamke bila kujishugulisha, kuna vitu ninafanya ambavyo wengi hawavioni ndiyo vinavyoniingizia pesa.

Lulu

Swali: Kumekuwa na miluzi mingi kuhusiana na ndoa yako kila kukicha mara inafanyika mwezi ujao, mara vikao vimeanza unazungumziaje hilo?
Lulu: Nafurahi kweli kusikia hizo habari, hivi mtu anawezaje kila siku anakutabiria ndoa? Sasa nazungumza mwenyewe kama Lulu, hakuna kitu kama hicho, kama ndoa amepanga Mungu kwa mtu ipoipo tu.
Swali: Baadhi ya mastaa wenzako wanasema kichinichini kama unajitenga , huonekani viwanja kama zamani au pale Leaders mlipokuwa mkikutana na wasanii wenzako, liko vipi hili?
Lulu: Jamani kila kitu kina wakati wake kabisa hivi mimi ni sehemu gani sijakanyaga au kiwanja gani sijaenda mpaka wengine waliweka kabisa bango niisiingie kwenye kumbi za starehe, hivyo kuna wakati mwingine unahitaji kuyabadili maisha yako kabisa.
Swali: Mara ya mwisho kutembelea kaburi la Kanumba ni lini?
Lulu: Unajua Watanzania wanapenda kuona mtu akifanya kitu lazima aweke kama matangazo, huwa natembelea kaburi lake kama moja ya ibada kwa wafu na hata kumuombea kanisani lakini ni vitu vyangu binafsi sio lazima kila mtu ajue nafanya hivyo.
Swali: Zamani kulikuwa na tetesi kuwa Dk. Cheni alikuwa anataka kukuoa hilo nalo vipi?
Lulu: (Kicheko) Hicho kitu hakipo kabisa.

Lulu.
Swali: Mastaa wengi siku hizi wamefululiza kupata watoto vipi wewe una mzuka na hiyo hali?
Lulu: Sipendi kufanya kitu kwa sababu watu fulani wanafanya, hakuna mtu ambaye hapendi mtoto, lakini naona bado muda wangu haujafika tu.
Swali: Zamani nilisikia umeokoka mpaka ukawa unatembea na Biblia kwenye pochi, vipi mpaka sasa upo hivyo?
Lulu: Kuokoka ni kumuabudu Mungu kwa kila jambo na bado nafanya hivyo, lakini pia kuhusu kutembea na Biblia sasa hivi hayo mambo mbona hayapo, ukitaka mstari wa Biblia unaupata kwenye simu tu.
Swali: Mara nyingi picha zako ukipiga inaonekana kama umehamia kwa shemeji vipi kuhusu hilo?
Lulu: Hapana bado niko nyumbani kwetu, naona ni mtazamo tu wa watu.
Swali: Vipi kuhusu shule bado unaendelea?
Lulu: Nasubiria kidogo nataka niendelee tena hivi karibuni ambapo nitakuwa nachukua Shahada ya Rasilimali Watu.
Ben Pol Baada ya Kujirusha na Kudakwa na Mashabiki

Swali: Tukija kwenye upande wa filamu ndiyo umeachana nako au vipi?
Lulu: Unajua watu unaweza kuwashangaa, mimi juzijuzi tu nimetoa filamu sasa sijui wanatakaje, lakini kwa vile kuna vitu vingine nafanya ndio maana huwezi kukomalia kitu kimoja tu na maisha yakaenda.
Swali: Siku hizi umebadilisha aina ya mavazi, umekuwa mara nyingi unavaa kiofisi zaidi kwa nini?
Lulu: Nimeamua kubadilika tu maana mtu asikukariri na kitu kimoja.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad