Manji Afunguka Mahakamani "Sitambui Kuvuliwa Udiwani Kama Ilivyotangazwa"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MFANYABIASHARA Yusuf Manji ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa hatambui kuvuliwa udiwani kama ilivyoandikwa kwenye vyombo vya habari.

Manji amesema anatambua kuwa yeye ni Diwani wa Mbagala Kuu na kwamba mahakama imuagize Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) awaambie Halmashauri ya Wilaya ya Temeke kwamba walimkamata na sababu za kutohudhuria vikao kwa miezi miwili ni kwa kuwa hana dhamana.

Ameyasema hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi. Amesema yeye amechaguliwa na wananchi na kwamba kama wanataka aende kwenye vikao, DPP aombe hati ya kumtoa gerezani ili akaudhurie vikao au wamuandikie barua yenye ajenda na kumbukumbu za vikao ili ajibu akiwa gerezani.

"Nimetumia zaidi ya milioni 70 kwa fedha zangu na sio za halmashauri kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wangu na nilikuwa nahudhuria vikao kabla sijakamatwa kwa kesi hii nzito.

Kwa kuwa naheshimu mahakama na kesi hii na kwa kuwa naheshimu mahakama hii na ukubwa wa kesi sikuomba dhamana," amesema Manji. Hakimu Shaidi amewataka upande wa mashitaka kufuatilia suala hilo na kwamba maombi yake yamechukuliwa.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad