AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Sugu aliyasema hayo wakati wa Ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa viti Maalum kupitia (CHADEMA) jiji la Mbeya Esther Mpwiniza aliyefariki dunia ghafla Septemba 16, mwaka huu kutokana na Shinikizo la damu.
Sugu alisema kwa kuwa jeshi la polisi limezuia ibada kwa ajili ya kumuombea Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu aliyejeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana yeye anaamini wanachama waliotangulia mbele za haki watafanya kazi hiyo kwa niaba ya wanachama.
Sugu aliendelea kusisitiza kuwa mbali na kupiga marufuku kufanya maombi pia serikali imekuwa ikiwazuia watu kwenda kwenye misiba ambapo alidai viongozi na wanachama walizuiwa kuhudhuria msiba wa aliyekuwa mbunge wa Moshi Mjini Marehemu, Philemon Ndesamburo.
“Naamini Kamanda wetu Esther saizi upo moja kwa moja na Malaika naomba ukamuombee Tundu Lissu apone haraka anyanyuke kutoka kitandani aendelee na kazi za ukombozi wa taifa letu, huku wametuzuia kufanya maombi lakini huko najua hawezi kufika kuwazuia,”alisema Sugu
Akizumzungumzia marehemu Mpwiniza Sugu alisema alikuwa ni mwalimu wa siasa na mpiganaji wa kweli kwa ajili ya maslahi ya wananchi wa jiji la Mbeya pamoja na chama na kwamba mchango wake umefanikisha ushindi wake kwa kiwango kikubwa. Amedai marehemu alikuwa ni ngao na mtu mwenye tabia ya kuwaunganisha wanachama na kuondoa tofauti ambazo zililkua zinatoa mwanya wa kuwepo kwa makundi ndani ya chama hicho.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK