Serikali ya Brazili Imeisamehe Tanzania Deni la Bilioni 445

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali ya Brazili Imeisamehe Tanzania Deni la Bilioni 445
Serikali ya Brazil imeisamehe serikali ya Tanzania deni lenye thamani ya bilioni 445 za kitanzania, ililokuwa inadaiwa na nchi hiyo.

Tarifa hiyo imetolewa leo na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas kwenye ukurasa wake wa twitter, na kufafanua kwamba deni hilo lilitokana na mkopo uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Morogoro-Dodoma, mwaka 1979 pamoja riba yake.

"Serikali ya Brazil imesamehe Tanzania deni la jumla ya dola za Kimarekani mil. 203 ambazo ni sawa na tsh bil. 445,deni hilo lilitokana na mkopo uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Morogoro-Dodoma mwaka 1979 pamoja riba," ameandika Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas
Msemaji wa serikali ameendelea kwa kusema kwamba kitendo hicho kimefungua milango iliyokuwa imefungwa kutokana na deni hilo, ambapo sasa makampuni ya Brazil yataweza kuja nchini na kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo.

Pia serikali imeshukuru Brazil kwa kitendo hicho na kuunga mkono jitihada za Rais John Pombe Magufuli za kuleta maendeleo ya nchi.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad