Shilole 'Mwanangu Anataka Kugundua Dawa ya Ukimwi'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msanii Shilole ameweka wazi kile ambacho watu wengi walikuwa hawafahamu kuhusu watoto wake, na kusema kwamba mambo yake ya mitandaoni hayawaathiri na badala yake wako vizuri darasani huku mmoja wao akiwa na ndoto kubwa ya kugundua dawa ya UKIMWI

Akizungumza na mwandishi wa habari Shilole amesema pamoja na kwamba yeye hajapata bahati ya kusoma, lakini watoto wake wako makini na shule huku akiwaonya na kuwasisitiza kuwa makini, kwani iwapo watafanya vibaya watakuwa wanamuangusha kutokana na anayoyapitia kwa ajili yao, hivyo wanazingatia ipasavyo kauli ya mama yao na kutojihusisha na mambo ya mahusiano yake.

"Wanangu hawana shobo na haya mambo, wanataka niwe na furaha, ndio maana hujaona watoto wangu wameniangusha kwenye masomo kwa vitu vya kusikia kwenye mitandao, ndio kwanza wanaongoza namba moja, namba mbili, nawaambia mkifanya blanda mnaniangusha mimi, mkifanya tukio mjue mnanizika, kwa hiyo watoto wangu wapo makini na masomo kuliko kitu chochote, huyu mmoja anasoma aje kuwa dokta ili aje agundue dawa ya UKIMWI, kwa nini uliletwa, na anafanya vizuri darasani", alisema Shilole.

Shilole ambaye ana watoto wawili wote wakiwa wa kike, anasema anajisikia faraja kuona watoto wake wanapa fursa ya kufanya yale ambayo yeye hakufanikiwa kuyafanya, ikiwemo kupata elimu bora ambayo anaamini itakuja kuwasaidia baadae kwenye maisha yao.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad