Yale Maneno na Makombora Bungeni ni Utamaduni wa Kibunge- Ndugai

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Yale Maneno na Makombora Bungeni ni Utamaduni wa Bunge- Ndugai
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amefunguka na kudai atahakikisha yeye na wabunge wanampa ushirikiano Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma aliyeapishwa leo baada ya kuteuliwa siku ya jana Septemba 10 mwaka huu.

Ndugai ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anatoa salamu za wabunge katika ghafla hiyo ya uapisho iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa bila ya kumsahau Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
"Sisi kama bunge tunawahakikishia ushirikiano mkubwa sana kwa kuhakikisha kazi za Mahakama zinaendelea kama zilivyo kikatiba na tutaheshimu sana. Yale maneno na makombora moja moja ya bungeni ni vitu vya kawaida, ndiyo utamaduni wa bunge",amesema Ndugai.
Aidha, Ndugai amesema Mahakama inamchango mkubwa kwa wananchi pamoja na taifa kwa ujumla kwa kuwa hicho ndicho chombo pekee kinachoweza kumtetea mnyonge kuweza kupata haki yake kutoka kwa waporaji.
"Kuwepo kwa Mahakama ndiyo usalama wetu, amani, kheri na matumaini ya mnyonge katika sheria na maamuzi ya Mahakama. Kwa hiyo tunakutakia kila la kheri katika kazi yako, tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu na tutakusaidia na kuomba msaada wako",amesisitiza Ndugai.
Kwa upande mwingine, Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma ameahidi kufanya kazi katika maadili ya kisheria pamoja na kurudisha imani ya wananchi kuhusiana na kupata misaada ya kisheria inayotolewa katika Mahakama mbalimbali ndani ya Tanzania.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad