Hans Poppe afunguka haya baada ya kiongozi wa Yanga kuchaguliwa kuiongoza Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti wa usajili wa klabu ya Simba Zacharia Hans Poppe amesema mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara (TPLB) Clement Sanga atende haki katika uongozi wake bila kujali kuwa yeye ni kiongozi wa Yanga.

“Yeye kuipenda Yanga hatumzuii kwa sababu ni mpenzi wa Yanga na kiongozi kule lakini atende haki asijipendelee”-Hans.

“Sasa hivi tunataka maendeleo ya soka sio mambo ya longolongo. Clement Sanga ni mtu ambae namfahamu nimezungumza nae mara kwa mara kwa mtazamo wake ni mtu ambae anapenda maendeleo nina imani atatekeleza wajibu wake vizuri.”

“Nimshauri tu kama kuna mambo anatakiwa ayasikilize wao kama rufaa basi wafanye ndani ya muda na kusimamia ratiba isibadilishwe mara kwa mara.”

Sanga ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa klabu Yanga amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara akimwangusha Ahmed Yahaya aliyekuwa madarakani awali kabla ya uchaguzi kufanyika.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad