Hii Hapa Safari ya Music ya Rosa Ree

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Hii Hapa Safari ya Music ya Rosa Ree
Staili ya kubinua midomo iliyokolea rangi nyeusi, mitindo ya nywele ya aina yake na vivazi vinavyoacha sehemu kubwa ya mwili wake vinamtambulisha vyema Rosa Ree.

Rapa huyo anayewakilisha kina dada katika gemu alitambulishwa na ngoma yake ya kwanza One Time akiwa tayari ameshaingia mkataba na lebo ya The Industry.

Mwanadada huyo ambaye jina lake halisi ni Rosary Robert Iwole kama wanamuziki wengine naye safari yake imeanzia mbali. Mwenyewe anasema haikuwa rahisi kama tembo kulitafuna bua…ilijaa mabonde na milima.

Mpaka sasa ameachia ngoma tatu ambazo zinakimbiza ambazo ni One Time, One Time remix ambayo alifanya na rapa kutoka Kenya, Khaligraph Jones, Up In The Air na kazi ya Mchaga Mchaga ambayo amewashirikisha mabosi zake kundi la Navy Kenzo.

Dili na The Industry?

“Muziki nilianza muda mrefu, yaani tangu nikiwa shule na tena nilikuwa naimba. Kuna ngoma kadhaa nilitoa ambazo nilikuwa naimba lakini hazikufanya poa,”

“Nilianza kuchana nikakuta watu wanapenda sana nikaamua kukaa humo. Mwaka 2015 nilienda kwa Nahreel kurekodi ngoma alivyonisikia tu alipenda sana. Baadae aliniomba niwe kwenye lebo yake nilifurahi sana kwanza halafu sikuamini lakini ikawa hivyo nikasaini hapo, mpaka sasa napiga mzigo,”

Mishe nyingine?

“Mimi nafanya biashara pia lakini mambo yangu mimi napenda kuyaweka kwa siri hivyo siwezi kusema ni biashara gani mpaka mambo yangu fulani yatimie,” aliongeza.

Nini kinafuata baada

ya Mchaga Mchaga?

“Baada ya Mchaga Mchaga kuna ngoma kali inakuja yani hapa nasubiri tu wakati uwadie kitu tukiachie, pia, nafikiria kutowachosha mashabiki zangu sababu nataka kuachia ngoma kali kwa kila kipindi fulani,” alisema.

“Na pia kuhusu video ya Mchaga Mchaga mipango bado ipo inafanyika ili kuja na kitu tofauti kama unavyojua Rosa Ree tangu nitoke kwenye upande wa video nikiri sijawahi kuzingua na hivyo najipanga kuja na jiwe kali sana.” Kolabo na Rapa wa Kenya?

“Aisee hii kolabo nikiri imenipa mafanikio makubwa sana,kwanza imeniongezea sana mashabiki kwa upande wa Afrika Mashariki kwa ujumla na mafanikio mengine ambayo siwezi kuyaweka wazi ila kiukweli nimepata mafanikio niliyotarajia,” Amesema.

Staili yake vipi?

Moja ya jambo kubwa ambalo mara kadhaa amekuwa akikumbana nalo ni watu kadhaa wamekuwa wakimkosoa hasa staili yake ya mavazi wakidai yapo nje ya maadili ya Kitanzania pamoja na matumizi ya maneno katika nyimbo zake ambayo yamejaa matusi sana.

“Mimi sifikirii hata kidogo kubadilika sababu eti kwa maneno ya watu sababu kuwa orijino ndicho kitu cha msingi halafu ukifuata kila kitu watu wanasema ni kazi sana kufanikiwa cha msingi mi sitobadirika bali nitazidi kuwa bora zaidi sababu naamini kuna watu wanapenda ninachokifanya,”

Watu wasichojua

kutoka kwake?

“Kuna vingi wengi hawajui kutoka kwangu, huwa wanaweka vitu vyao kutokana na namna wanavyoniona, lakini kiukweli mimi napenda sana sana watoto na situmii kilevi chochote kuna watu huwa hawaamini lakini ukweli ndio huo,”

Kama si Muziki basi angekuwa anafanya nini?

“Ningekuwa daktari aisee kama sio muziki maana ni kitu ambacho kilikuwa akilini mwangu kwa hiyo kama nisingekuwa nafanya muziki basi ningekuwa nachakarika na wagonjwa Hospitalini,”

Shoo ambayo hatokuja

kusahau.

“Sitokuja kusahau shoo ya “Castle Lite Unlock” ki ukweli shoo nyingi huwa napata shangwe sana ila hiyo shoo nakumbuka nilipafomu wimbo wa Mchaga Mchaga ambao ulikuwa bado haujatoka na watu walikuwa wakiitikia ilinipa sana nguvu asikwambie mtu,”

Vitu ambavyo hapendi

kuja kuvifanya kabisa

“Kitu ambacho sifikiri kabisa kuja kufanya ni siasa,mimi sipendi kabisa siasa na sifikiri kabisa sijui kwa mbele itakuaje ila akili yangu inaniambia hivyo kwamba Rosa Ree siasa wewe kwako haipo,”

Albamu na Mixtapes

(Kanda Mseto) vipi?

“Mipango ipo sema nafikiri bado mashabiki zangu wanahitaji singo zaidi ili kuwatengenezea nafasi ya kuja kufurahia albamu yangu ila mipango ipo na pindi itapowadia watu wataona.”

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad