AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wikiendi hii Irene Uwoya kupitia ukurasa wake wa Instagram amekuwa bize kuposti picha zake akiwa ndani ya shela huku akimshukuru Mungu kwa kufanikisha zoezi hilo.
Licha ya Irene Uwoya kutomtaja mwanaume, marafiki zake wa karibu wamempongeza na kumtaja mwanaume huyo kuwa ni Dogo Janja.
Mtu wa kwanza kutoa pongezi kwa Irene Uwoya ni Mtangazaji wa Clouds TV, Zamaradi Mketema ambapo amemtaja Dogo Janja kwenye pongezi hizo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika “Hongera Sana kwa NDOA mpenzi wangu, mwanzo nilihisi ni movie lakini sasa nimeamini.. MUNGU awatangulie katika hili mlilolifanya @ireneuwoya8 @dogojanjatz kila la kheri INSHA’ALLAH!!”
Hata hivyo licha ya kuzagaa kwa taarifa hizo mitandaoni kuwa wawili hao wamefunga ndoa bado Dogo Janja hajatoa taarifa yoyote kuhusu tetesi hizo.
Watu wa karibu na Dogo Janja wamekanusha taarifa hizo lakini Madee kwenye mahojiano yake mafupi na Bongo5 amethibitisha kuwa mwanaye Dogo Janja amefunga ndoa na harusi yake imefanyika Ijumaa ya wikiendi hii.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK