Maandamano ya Kupinga Kujitenga kwa Catalonia Kufanyika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Maandamano ya Kupinga Kujitenga kwa Catalonia Kufanyika
Wale wanaopinga juhudi za jimbo la Catalonia kujitenga leo wamepanga maandamano makubwa huko mjini Madrid wakisema Uhispania ni taifa moja na hawataki ligawanyike.
Sintofahamu hiyo imetokana na kufanyika kwa kura tata ya juzi ambapo Catalonia ilisema kura ndiyo ingeamua iwapo wajitenge .

Japo wanasema asilimia kubwa ya waliopiga kura waliunga mkono, bado hawajatangaza uhuru wao wala hakuna dola yoyote ya nje na ndani ya Uhispania inayoitambua.
Utawala wa serikali kuu ulitumia nguvu na mbinu tofauti tofauti kujaribu kuzuia kura hiyo .
Mzozo huo umesababisha wasiwasi mkubwa sio tu wa kisiasa bali pia wa kibiashara.
Mapema leo benki ya pili kuu Caixabank, imetangaza kuondoa makao yake makuu kutokana na wasiwaasi unaoendelea kuligubika eneo hilo

Shirika la fedha dunia ,IMF limesema mzozo huo unaharibu mazingira ya uwekezaji wa Catalonia.
Ni dhahiri pande zote mbili na hata jamii ya kimataifa zingependa kuona mzozo huo umesuluhishwa kwa majadiliano lakini bado hamna dalili zozote kwamba yatafanyika hivi karibuni.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad