Sekta Binafsi Zina Hali Mbaya- Simbeye

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Sekta Binafsi Zina Hali Mbaya- Simbeye
Mkurugenzi wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) Bwana Godfrey Simbeye, amesema sekta binafsi sasa hivi zinapitia kwenye wakati mgumu kutokana na kodi ambazo TRA wameziweka, kitu ambacho kinaweka mazingira magumu ya kazi za uzalishaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye
Bwana Simbeye ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba licha ya serikali kuweka jitihada zake za kuimarisha sekta hizo, lakini kumekuwa na changamoto kubwa inakuja kwenye utaratibu usiofaa wa ukasanyaji kodi.
“Serikali kwa juhudi zake imeendelea kutengeneza mazingira mazuri ya biashara, kama kurekebisha njia za usafirishaji ikiwemo reli na viwanja vya ndege, lakini suala la kodi limekuwa ni tatizo, malalamiko mengi ya sekta binafsi yanatoka kwa namna ambavyo TRA wanakusanya kodi, ni kero kubwa, imekuwa kwa mwezi mmoja taasisi binafsi inaweza ikatembelewa na timu ya TRA tatu na zote zikaja na makadirio tofauti, kwa hiyo hilo suala tunatakiwa tuliangalie”, amesema Bwana Simbeye.
Bwana Simbeye ameendelea kwa kusema kwamba changamoto nyingine ambazo sekta binafsi zinapitia kwenye kipindi hiki ambacho uwekezaji unakua, ni pamoja na kukosa mikopo, kutokana na hali ya mabenki ilivyo kwa sasa.
“Uwekezaji mpya unakua Tanzania, hata kwenye kituo cha uwekezaji project mpya zimeongeneka, lakini uwekezaji wa ndani bado haujakuwa sana kwa sababu hali ya kukopesha kwenye sekta binafsi bado haijawa nzuri, bado hatujaona dalili nzuri ya ukopeshaji wa mabenki kwenda sekta binafsi, ingawa serikali imekuwa ikiendelea kutoa dhamana ya serikali, lakini kwa upande wa sekta binafsi bado”, amesema Bwana Simbeye.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad