Spika Ndugai amshukuru Dk Kashililah kwa Utumishi Uliotukuka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Spika Ndugai amshukuru Dk Kashililah  kwa Utumishi Uliotukuka
Spika wa Bunge, Job Ndugai amemshukuru aliyekuwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah kwa utumishi uliotukuka.

Ametoa shukrani hizo leo Jumatatu Ikulu jijini hapa baada ya Rais John Magufuli kuwaapisha mawaziri, manaibu na Katibu wa Bunge mpya, Stephen Kagaigai.

Spika Ndugai pia amewakaribisha mawaziri, manaibu na katibu huyo bungeni mjini Dodoma.

“Ninyi mnatokana miongoni mwetu katika nyumba ile ya wabunge. Rais ameona awape nyadhifa hizi, kubwa na la kipekee nimkaribishe Katibu wa Bunge mpya Kagaigai na kipekee nimshukuru Dk Kashililah, asante sana kwa utumishi uliotukuka hatutakusahau,” amesema.

Amesema timu ya Baraza la Mawaziri ana imani nayo kwamba itafanya kazi vyema. Baada ya kuapishwa leo, watakutana katika kikao cha Baraza la Mawaziri.

“Mje Dodoma mmejiandaa, hii miaka miwili ya mwanzo walikuwa wanajifunza funza, sasa tukienda Dodoma itakuwa ni kazi tu,” amesema Spika Ndugai.

Wakati huohuo, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amesema kile walichokitamka katika kiapo cha uadilifu wanapaswa kukizingatia kwa kufuata utaratibu wa kisheria na Katiba ili kuepusha migongano.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad