Taharuku Yatanda Baada ya Mwanamke Mwizi wa Nyanya Kushindwa Kutua Tenga Yawalazimu Polisi Kutumia Mabomu Kuwatawana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Taharuku Yatanda Baada ya Mwanamke Mwizi wa Nyanya Kushindwa Kutua Tenga Yawalazimu Polisi Kutumia Mabomu Kuwatawana
Uvumi kuhusu mwanamke mwizi wa nyanya kushindwa kutua tenga umesababisha polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi mjini Mbalizi.

Hali ya taharuki imewakumba wananchi wa mji mdogo wa Mbalizi leo Jumatano baada ya mtu au watu wasiojulikana kuvumishwa kuwa mwanamke huyo baada ya kushindwa kutua tenga alikimbilia kituo cha Polisi Mbalizi kuomba msaada.

Uvumi huo ulieleza kuwa, mwanamke huyo aliimba nyanya sokoni Mbalizi.

Katika tukio hilo jana mchana Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi waliovamia kituo hicho ili kumuona mtuhumiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga amesema uvumi huo ulienezwa na watu au mtu asiyejulikana kwamba kuna mwanamke aliiba tenga la nyanya sokoni Mbalizi lakini alipojaribu kulishusha kutoka kichwani ilishindikana, hivyo akaamua kwenda kituo cha polisi kuomba msaada.

“Wakati wa taharuki kama ile kila mtu anakuwa na tabia na nia yake, ndiyo maana imelazimika kutumia nguvu kidogo kuwanyamazisha watu kwa mabomu. Ule ni uvumi tu ambao hata hatujamfahamu aliyeeneza alikuwa na mlengo gani kwa kuwa hakuna tukio kama hilo,” amesema.

Kamanda Mpinga amesema sasa hali ni shwari na wananchi wameelimishwa wakaondoka kwenda sehemu zao za biashara na shughuli nyingine.

Mwenyekiti wa Soko la Mbalizi A ambako kituo cha polisi kipo, Geofrey Msigwa amesema hakuna kitu kama hicho bali naye aliona watu wengi wakielekea kituoni jambo lililosababisha polisi kuwatawanya kwa mabomu.

Amesema, “Hii ni hatari kwa mtu kusikia jambo bila kulifanyia utafiti na kuanza kulizusha bila kutambua athari inayoweza kutokea.”

Amelaani kitendo hicho akisema kinahatarisha usalama na amani.

Pia, amewaonya watu kutokimbilia vitu ambavyo ni vya kusikia bila kuvifanyia uchunguzi kwa kuwa inaweza kuwagharimu.

Msigwa amesema hawana taarifa za wizi huo na wanashangazwa na uvumi huo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad