Walioshindwa Uchaguzi CCM Wapinga Matokeo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Walioshindwa Uchaguzi CCM Wapinga Matokeo
Matokeo ya uchaguzi wa Wenyeviti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), yamepingwa katika wilaya nne kati ya saba za Mkoa wa Mwanza kutokana na madai ya kugubikwa na vitendo vya rushwa na ukiukwaji wa kanuni za uchaguzi.

Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Acheny Maulid alitaja wilaya ambazo matokeo yake yamewekewa pingamizi kuwa ni Magu, Nyamagana, Misungwi na Sengerema.

Aliwataja wenyeviti ambao ushindi wao unapingwa ni Zebedayo Athumani kutoka Nyamagana, Daudi Gambadu (Misungwi), Zabloni Makoye (Magu) na Agostine Makoye wa Sengerema.

“Vikao husika vitakutana kujadili na kuamua pingamizi hizo kwa mujibu wa katiba na kanuni za uchaguzi ndani ya chama,” alisema Maulid.

Uchaguzi wa wenyeviti wa wilaya wa CCM katika wilaya zote saba za Mkoa wa Mwanza ulifanyika Oktoba 5. Wenyeviti wengine waliochaguliwa ambao hawajawekewa pingamizi hadi juzi ni Peter Muyanga kutoka Kwimba, Ally Mambile (Ukerewe) na Nelson Mesha wa Ilemela.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad