Waziri Jafo Aagiza Wanafunzi Kufanya Mitihani ya Mchujo Kabla ya Kuvuka Darasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri Jafo Aagiza Wanafunzi Kufanya Mitihani ya Mchujo Kabla ya Kuvuka Darasa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo ameagiza wanafunzi wa shule za Serikali kufanya mtihani wa mchujo kabla ya kupandishwa vidato.

Pia, amesema hatapanga ada elekezi kwa shule binafsi bali watapunguza wenyewe.

Jafo ametoa kauli hiyo leo Jumatano mjini Dodoma alipozungumza na wafanyakazi wa Tamisemi.

Ametoa kauli hiyo akisema shule kongwe za Serikali zimekuwa ‘zikikimbizwa’ na za binafsi.

"Naagiza kuanzia leo, lazima wanafunzi wa shule za Serikali wafanye mitihani mara mbili, mwezi wa sita na mwisho wa mwaka ili kuwachuja wa shule zenye vipaji maalumu na kuwarudisha shule za kawaida za Serikali, vinginevyo ndiyo maana tunafanya vibaya wakati wote," amesema.

Amesema katika mchujo huo, wanafunzi watatolewa kutoka shule kongwe na kupelekwa za vipaji maalumu na vivyo hivyo kutoka vipaji maalumu kwenda shule kongwe.

Kuhusu ada kwa shule binafsi amesema si jukumu la Serikali bali wanataka kuboresha shule zake ili watu na taasisi binafsi zikose wanafunzi.

"Mheshimiwa Kakunda (Joseph –Naibu Waziri Tamisemi) nakuagiza kuanzia leo maana wewe ndiyo nimekukabidhi jukumu la elimu, nataka mtihani wa 2019 shule za vipaji zote 22 ziongoze mtihani wa Taifa na shule binafsi ziwe nyuma, lakini tuongoze kwa halali si ubabaishaji hapo ndipo shule binafsi za makanjanja zitajifuta zenyewe," aliagiza Jafo.

Wakati huohuo, Jafo amewaagiza watendaji katika idara ya elimu kushughulika na wakuu wa shule kongwe zote ili kuona kama bado wana sifa za kuendelea kuwa wakuu wa shule au kuwaondoa wanaoonekana kushindwa kazi.

Kuhusu watendaji wa Tamisemi amesema hataki mambo matatu wizarani hapo ambayo ni ulegevu, mazoea na kutojali muda ambayo amesema ni adui wa mafanikio.

Naibu waziri, Kakunda amesema hana shaka na kazi aliyopewa akiahidi kuifanya kwa kutumia weledi na uzoefu wake ili kuibadilisha Tamisemi.

Kakunda ambaye kabla ya kuwa mbunge alikuwa mkurugenzi Wizara ya Maji amesema mipango mingi anaijua lakini akaomba ushirikiano kwa watumishi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad