AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Maandalizi yameanza katika uwanja wa kitaifa wa michezo katika mji mkuu wa Harare ambapo hafla hiyo itafanyika.
Mwandishi wa maswala ya kidiplomasia Judith Makwanya amesema kuwa kiongozi anayeondoka anatarajiwa kukagua gwaride akitoa kwaheri huku kiongozi mpya akilijulisha jeshi katika sherehe hiyo ya gwaride.
Tayari waziri wa Uingereza barani Afrika Rory Stewart amewasili nchini Zimbabwe mapema kulinga na chombo cha habari cha AFP.
Mugabe: ''Naombewa nife''
Mugabe atakumbukwa kwa mabaya
Rais Robert Mugabe amejiuzulu
Afisa huyo amewasili tayari kuhudhuria kuapishwa kwa rais mpya siku ya Ijumaa.
Bwana Sterwart anatarajiwa kukutana na viongozi wa kisiasa na wale wa kibiashara pamoja na makundi ya haki za kibinaadamu na mashirika yasiokuwa ya kiserikali kulingana na waziri wa maswala ya kigeni nchini Uingereza.
Ametaja mabadiliko hayo ya kihistoria kuwa wakati muhimu baada ya utawala mbaya wa rais wa zamani Robert Mugabe.
Uingereza inataka kuwa mshirika wa kweli wa raia wa Zimbabwe wakati huu ambao wanaanza mwanzo mpya, bwana Stewart aliambia AFP
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK