Polisi Wafanya Upekuzi Makao Makuu ya ACT Wazalendo, Waondoka na Nyaraka, Vifaa vya Kielektoniki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Polisi Wafanya Upekuzi Makao Makuu ya ACT Wazalendo, Waondoka na Nyaraka, Vifaa vya Kielektoniki
Jeshi la Polisi limefanya upekuzi Makao Makuu ya Chama cha ACT- Wazalendo na kuchukua nyaraka, vifaa vya kiilektonikia vilivyotumika kuandaa taarifa ya kusinyaa kwa uchumi wa nchi.

Upekuzi huo umefanyika leo mchana muda mfupi baada ya Zitto kwenda kuripoti Kitengo cha Uhalifu wa Makosa ya Kifedha Kamata jijini Dar es salaam na kutakiwa kurejea tena Novemba 21.
Taarifa iliyotolewa jioni hii na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Ado Shaibu amesema polisi walifika ofisini hapo saa 6 mchana na wameondoka mida ya saa 10 na wamechukua flash, laptop (kompyuta mpakato) na nyaraka ambazo ni taarifa kwa umma iliyotolewa kupitia wanahabari.
Ado amesema kwamba “Wamesema watakwenda kufanyia kazi vifaa hivyo na watavirejesha haraka ila hawajasema hasa ni lini," ameongeza
Mapema leo Jeshi hilo la polisi lilishikilia simu ya mkononi ya Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe kwa upelelezi huku yeye akisema mawasiliano aliyokuwa akiyafanya yamezingatia uhuru ulipo katika Katiba.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad