AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rais amesema hayo mapema leo wakati akihotubia wananchi waliojitokeza kwenye ufunguzi wa Hospitali na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila.
“Nikiwa Waziri Mheshimiwa Pinda alinipinga kuhusu kubomoa jengo la TANESCO lakini kwa sasa hawezi kwasababu Mimi ndiye Rais, nilikaa kimya kwasababu ya kuogopa kufukuzwa”, amesema Rais Magufuli.
Aidha rais ameongeza kuwa Jengo hilo lazima libomolewe hata kama nusu yake ndio ipo kwenye hifadhi ya barabara basi itolewe kama ni lote basi liondolewe pamoja na jengo la wizara ya maji hivyo hivyo kwasababu sheria ni msumeno.
Pia rais amesema wakazi wa Kimara ambao nyumba zao zimebomolewa hawatalipwa fidia kwasababu zilikuwa ndani ya hifadhi ya barabara.
“Mwaka 1997 wakati nikiwa naibu waziri wa Ujenzi nilikuja Kimara wakati wa kubomoa eneo la Kimara hadi Ubungo nilisema hata waliobaki wapo ndani ya hifadhi ya barabara hivyo wasiendelee na ujenzi”, amesema Rais Magufuli.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK