Uongozi Ubungo Plaza Limitedi Wafunguka Kuhusu Kufungiwa kwa Hotel ya Brue Pearl

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Uongozi Ubungo Plaza Limitedi Wafunguka Kuhusu Kufungiwa kwa Hotel ya Brue Pearl
Uongozi wa Ubungo Plaza Limited umesema mpangaji wake, hoteli ya Blue Pearl alikoma kulipa kodi ya pango tangu Mei, 2014.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 9,2017, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Ubungo Plaza, Harun Mgude amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kushinda kesi Mahakama ya Ardhi.

"Blue Pearl amekuwa mpangaji wetu tangu mwaka 2006 na mkataba wake ulikuwa wa miaka 15 ambao ungeisha 2021. Alikuwa akilipa vizuri lakini tangu Mei 2014 aliacha kulipa," amesema Mgude.

Amesema kutokana hilo walikwenda kufungua kesi Mahakama ya Ardhi na Blue Pearl wameshindwa, hivyo kutakiwa kulipa au kutoka ndani ya jengo.

"Kama mnakumbuka tuliwahi kumtoa na akarudi kwa amri ya Mahakama ili kupisha kesi kuendelea, lakini Novemba 3,2017 kesi iliisha na ameshindwa na kutakiwa kulipa deni la Sh5.7 bilioni," amesema.

Amesema uongozi wa Blue Pearl umeomba kufanya kikao Jumatatu Novemba 13,2017 ili kujadili jinsi ya kulipa deni hilo.

"Baadhi ya wateja wamehamishiwa hoteli nyingine sijui ni wapi. Ila ieleweke kuwa robo tatu ya mali zilizokuwamo Blue Pearl ni za Ubungo Plaza Limited kama vile fenicha na vitu vingine," amesema Mgude.

Uongozi wa hoteli hiyo ulikuwa ukishughulikia kuwahamisha wateja na haukuwa tayari kuzungumzia suala hilo.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad