AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, imemsainisha nyota huyo mkataba wa miaka miwili na ataanza kuitumikia timu hiyo pale ligi itakapoendelea baada ya kupisha michuano ya Kombe la Chalenji.
Mkomolwa ambaye alifanya vizuri na Serengeti Boys kwenye michuano ya Afrika iliyofanyika, Gabon mwaka huu,anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Yanga kwenye dirisha hili dogo.
Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, akizungumza na gazeti hili jana, alithibitisha 'kinda' huyo kusajiliwa na Yanga.'Ni kweli Mkomolwa amejiunga na sisi..., na hii ni katika kuboresha kikosi chetu," alisema Saleh.
Katika hatua nyingine, Saleh, aliema kuwa kocha wa timu hiyo, George Lwandamina, ametoa mapumziko ya wiki moja kwa wachezji wake.
Alisema wachezaji wa timu hiyo wataendelea na mazoezi Jumatatu ijayo kwenye Uwanja wa Uhuru.
"Unajua baada ya ligi kusimama, kocha ameamua kuwapa wachezaji ambao hawamo kwenye vikosi vya timu za Taifa mapumziko ya wiki moja, tutaanza mazoezi Jumatatu ijayo,"alisema Saleh.
Yanga inawachezaji kwenye vikosi vya timu ya Taifa ya Tanzania Bara 'Kilimanjaro Stars' na ile ya zanzibar 'Zanzibar Heroes' ambazo zote zitashiriki michuano ya Chalenji inayoanza Desemba 5, mwaka huu nchini Kenya.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK