AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Harmorapa akiongea kwenye kipindi cha eNewz cha EATV amedai kuwa baada ya kuhangaika kwa marafiki zake Wema Sepetu na kugonga mwamba aliamua kwenda kwa babu (mganga) ambapo amedai kwa mara ya kwanza aliambiwa apeleke kuku mweupe, na alipeleka huyo kuku lakini aliporudi mjini Dar es Salaam mambo yake yakawa bado vile vile.
"Nimemuendea kwa babu Wema Sepetu mara tatu, nilipokwenda mara ya kwanza niliambiwa nipeleke kuku mweupe, nikapeleka zangu yule kuku mganga akafanya yake lakini niliporudi mjini sikuona mabadiliko yoyote yale, nikamfuata tena babu akaniambia nipeleke vitu vingine viwili ambavyo hapa nashindwa kuvisema" alisema Harmorapa
Harmorapa aliendelea kufunguka jinsi ambavyo amehangaika kulitafuta penzi la Wema Sepetu na kudai ilifika wakati aliambiwa apeleke mchanga wa unyayo wa Wema Sepetu au mchanga ambao mwanadada huyo ametemea mate, kitu ambacho Harmorapa amedai kilikuwa kigumu sana kwake kwa sababu hapati nafasi ya kukutana live na Wema Sepetu.
Hata hivyo Harmorapa kwa sasa amesema amemwachia Mungu juu ya jambo hilo baada ya kuona harakati za kwa mganga wa kienyeji zinakwama.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK