Kinana Apewa Shavu Hili na Rais Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kinana Apewa Shavu Hili na Rais Magufuli
Katibu mkuu wa Chama  Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana leo ameteuliwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Rais John Pombe Magufuli  kuendelea kuwa katika nafasi yake kwa kipindi kingine.


Akiongea katika mkutano wa 9 wa Chama hicho unaoendelea mkoani Dodoma amemshukuru kwa kazi yake nzuri  kwa muda wote ambao amekuwa  katika nafasi hiyo huku akiweka wazi kuwa ni lazima aendelee kufanya nay kazi kwasababu ameridhishwa na utendaji wake wa kazi.

''Namshukuru ndugu Kinana kwa msaada wake mkubwa alionipa kwa kipindi chote hicho nafikiri  anafaa kuendelea kuwa katika nafasi hiyo kwa kipindi kingine,'' amesema Magufuli. Kauli ya Rais Magufuli inaondoa tetesi zote zilizokuwa zinadai kuwa Kinana ameandika barua ya kuomba kujiudhuru katika nafasi yake kwa kilichodaiwa kuwa haridhishwi na utendaji wa Mwenyekiti wake Rais Magufuli.

Baada ya kupata nafasi  hiyo Abdulrahman Kinana amemshukuru Rais Magufuli kwa kumuamini pamoja na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kukijenga chama hicho pamoja na nchi  kwa ujumla.

Kinana aliwahi kuwa mtumishi wa Jeshi la Tanzania kwa miaka 20 pamoja na kuwa Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki mwaka 2001 hadi 2006, amechaguliwa kuwa Katibu mkuu wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM), tangu 2012.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad