Polisi Yachukua Magari Yake Yaliyokwama Bandarini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Polisi Yachukua Magari Yake Yaliyokwama Bandarini
Hatimaye magari 50 ya Jeshi la Polisi yalikuwa yamekwama Bandari ya Dar es Salaam tangu mwaka 2015 yamechukuliwa wiki iliyopita.

Novemba 26 mwaka huu, Rais John Magufuli alitembelea Bandari ya Dar es Salaam na kukuta magari ya polisi yakiwa yamekaa bandarini kwa muda mrefu wakati yalitakiwa kukaa hapo kwa siku 21.

Rais Magufuli alimwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi, (IGP) Simon Sirro kuyachukua ili yakafanye kazi iliyokusudiwa.

Leo Jumanne, Msemaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Janeth Ruzagi amesema magari hayo yameshachukuliwa na polisi.

Alisema mamlaka hiyo na polisi wamefikia makubaliano na kuyachukua magari hayo na sasa yameshaondolewa bandarini.

Akizungumzia magari ya polisi, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa amesema ni kweli wameyachukua magari hayo.

Amesema walitii agizo la Rais na kufanya mazungumzo na bandari na sasa wameshayachukua kwa ajili ya kazi mbalimbali za polisi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Something not correct here. No one in the police department knew. Or someone ordered and sold to police.Tell us the truth. Whose business is this.

    ReplyDelete

Top Post Ad