Tuache siasa kwenye ujenzi: Majibu ya nyufa hizi, yatolewe na The Professionals, AQRB, ERB, CRB, na sio mtuhumiwa TBA!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Baada ya kuthibitishwa hizi nyufa ni za kweli kwenye hostel za UDSM, TBA imetoa ufafanuzi nyufa hizi kitu cha kawaida, hivyo wananchi tusiwe na wasiwasi.

Kwa vile sisi sii wataalamu, TBA ndio wataalamu, kunapotokea tuhumu kama hizi, na mtuhumiwa ni TBA kuwa amejenga chini ya kiwango, au amelipua, then mtu sahihi wa kusema nyufa hizo ni kawaida sio mtuhumiwa TBA, bali sasa, the assurances kuwa all is well, nyufa hizo ni kitu cha kawaida, utolewe na the professionals kuanzia kwa Bodi ya AQRB wathibitishe ile bilioni 10 inaweza kujenga majengo hayo na yakawa madhubuti, ERB wawathibitishe TBA waliwatumia watu sahihi, na CRB na mamlaka za ukaguzi wa ubora wa majengo ndio watuthibitishe kuwa walikagua ujenzi step by step na kujiridhisha, ndipo TBA waruhusiwe kuziba nyufa hizo,tena tuombe Mungu, nyufa zenyewe ziishie kwenye kuta tuu, kama kuna nyufa hadi kwenye structural, yatakuwa mengine!, vinginevyo sio tusipoziba ufa, tutatenga tuu ukuta, bali tunaweza kuja kujenga ukuta wa damu!.

Tanzania ili tupate maendeleo ya kweli, ni lazima tuache kuingiza siasa kwenye kila kitu!, ujenzi wa majengo hayo uligubikwa na siasa nyingi, ili kukidhi matakwa ya kisiasa, yametumia gharama ndogo za ajabu, ili kuonyesha jinsi tunavyoibiwa kwenye ujenzi.

Tufanyeni siasa kwenye siasa, lakini tusiingize siasa kwenye kazi za watu just for the sake of political capitalization, hatma ya hizi hostels, utatoa funzo moja zuri sana kuhusu kuingiza siasa kwenye tasnia ya ujenzi.
Sometimes cheap is expensive, huu ni ufa tuu, ila ulivyo mkubwa, hii ni dalili hapa mbele ya safari tutakuja kujenga ukuta, hala hala tuu, usiwe ukuta wa damu!

By Paskali Mayalla/JF
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad