AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jeshi hilo lilimchukua mchungaji huyo na familia yake ya watu watano na kuwakabidhi Holili upande wa Kenya, lakini Serikali ya Kenya ikakataa kuwapokea.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, mchungaji huyo alisema licha ya Mahakama kutoa zuio la muda kwa jeshi hilo na mwanasheria mkuu wa Serikali, bado jeshi hilo linaendelea kuwabugudhi.
Mkuu wa uhamiaji mkoa wa Kilimanjaro, naibu kamishina wa uhamiaji (DCI), Albert Mwelamila alisema asingependa kuzungumzia malalamiko ya mchungaji huyo kwa vile ameshakwenda kortini.
“Ushahidi tuliokusanya unaonyesha si raia wa Tanzania na wamezaliwa Kenya sasa kwa sababu kuna zuio la Mahakama tunaheshimu hilo lakini tuna uhakika kuwa si raia wa Tanzania,” alisema Mwelamila.
Zuio la muda lililotokana na maombi namba 46/2017, lilitolewa Desemba 18 mwaka huu na Jaji Aishiel Sumari, ambaye aliwazuia wadaiwa kuwakamata wadai hadi shauri la msingi litakaposikilizwa.
Kwa mujibu wa amri hiyo, Jeshi la Uhamiaji na Mwanasheria mkuu wa Serikali, wamezuiwa kuwakamata mchungaji huyo na familia yake, ambayo ni pamoja na mkewe, Redempter Francis.
Hata hivyo, mchungaji huyo alidai kwamba siku moja baada ya kutolewa kwa zuio hilo, maofisa hao walikwenda nyumbani kwake eneo la Majengo kwa nia ya kuwakamata.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK