AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Habari zilizopatikana kutoka kwa mmoja wa ndugu zake zimesema waliofanya hivyo walikuwa wamelenga kulichukua fuvu lake. Kaburi lake lilikuwa likilindwa na polisi kuzuia watu wasilifukue na kuchukua fedha ambazo zilitupwa ndani ya kaburi hilo na marafiki zake waliokuwa wanajiita “kundi la matajiri”.
“Nilikuwa nikipita karibu na kaburi majira ya saa saba mchana na niliona shimo kwenye kaburi la Ssemwanga. Nilisogea karibu kuona nini kilikuwa kimetokea,” alisema Ali Wamala, mmoja wa ndugu wanaoishi nyumbani hapo. Hata hivyo, alidai kwamba huenda waganga wa kienyeji walikuwa nyuma ya njama za kuufukua mwili wa Ssemwanga.
Polisi walililinda kaburi hilo kwa zaidi ya mwezi mzima. Naye Naibu Mkuu wa wilaya hiyo, Yahaya Were, amesema upelelezi umeanza na watuhumiwa watakaokamatwa watafikishwa mahakamani. “Hili ni suala la usalama na polisi wameanza uchunguzi dhidi ya watu wanaotaka kuharibu amani ya wafu,” aliongeza Were.
Tangu kuzikwa kwa Ssemwanga, ndugu zake walikodi walinzi kulinda kaburi hilo lakini habari za kuaminika zimesema walishindwa kuwalipa mishahara yao kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa. Inasemekana walinzi hao mwezi wa kwanza walilipwa Sh. 600,000 mbali na kwamba walikuwa wamekubaliana kuwalipa Sh. milioni moja.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK