Waziri Mhagama Atoa Agizo Hili Loliondo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waziri Muhagama Atoa Agizo Hili Loliondo

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Watu wenye Ulemavu ) Mhe. Jenista Mhagama ameitaka (MIVARF) kuongeza thamani ya biashara za mifugo wilayani Longido.

Waziri Mhagama ametoa agizo hilo baada ya kukagua soko la kimkakati lililojengwa na serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Program ya miundombinu ya masoko, uongezaji thamani na huduma za kifedha vijijini (MIVARF).
Soko hilo lililopo wilayani Longido litawanufainisha wananchi wapatao 142,000 wa wilayani humo ambao asilimia 95 ni wafugaji na huzalisha bidhaa zitokanazo na mifugo.
Soko hilo la kimkakati limeingiza mapato ya jumla ya kiasi cha shilingi milioni 106 kwa mwaka 2016/17, na kusaidia wilaya hiyo kuweka rekodi ya kuingiza mapato ya bilioni 1.3 kwa mwaka kitu ambacho hakikuwahi kutokekea hapo awali.
MIVARF ni Programu ya Miundombinu ya Masoko na Huduma za kifedha vijijini, iliyobuniwa mwaka 2011 na serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na inatekelezwa katika mikoa 29 nchini.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad