AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hatua hiyo imekuja baaada ya timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) kutinga hatua ya fainali ya michuano ya CECAFA Senior Challenge 2017 inayoendelea nchini Kenya.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Facebook Zitto amefunguka ya moyoni akitaka ZFA iwe mwanachama wa shirikisho la soka la kimataifa FIFA pamoja na lile la Africa CAF angalau kwa miaka mitano na inaweza kupiga hatua ambazo TFF imeshindwa.
“Kama hatutaki Zanzibar kuwa Mwanachama wa FIFA kama ilivyo Scotland. Tuseme kwa miaka 5 ijayo kuanzia mwaka huu ZFA ndio mwanachama FIFA na CAF ili TFF ipate muda wa kujipanga. Ndani ya hiyo miaka 5 nawaambia Zanzibar itakwenda AFCON na hata Kombe la Dunia. #MsemaKweliMpenziWaMungu”, ameandika Zitto Kabwe.
Zitto ametoa mfano kuwa Zanzibar ingepata uanachama kamili wa FIFA kama ilivyo kwa nchi za Scotland pamoja na Wales ambazo pia ni nchi dada za taifa la Uingereza lakini zinatambuliwa na FIFA kama mataifa wanachama huku Uingereza ikitambulika kama England.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Mhhhh . Zitto amwandikia sepp Blater
ReplyDeleteMajibu umeambiwa lini yatakyja kwako au kea Mwakyembe?
Mwakyembe...Dogo anajalibu bahati yake kwako.
ReplyDeleteAlivyo wacha playstation kuchaji akaenda nchini twits ili ajalibu kazi za wizala yako.
Sijui kava ikiwa au umemtolea nje
" Zitto Kabwe Akiombea Uanachama wa FIFA Chama Cha Soka Zanzibar (ZFA)"
ReplyDeletehaya maombi yamepelekwa nchi gani ?
haya maombi amepelekewa Nani?
haya maombi yanatarajiwa kujibiwa na baraza lipi?
haya maombi ni genuine au Feki?
Huyo Dogo kwa hivi sasa Anarepresent Wizara Gani katika haya Maombi na Waziri wake ni Nani?