AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
ASKARI wa Uingereza aliyewahi kuwa shujaa wa vita nchini Afghanistan, hivi majuzi alimbaka askari mwenzake wa kike baada ya kujigamba kwamba alikuwa na uume mrefu.
Haya yalisema mahakamani ambapo Luteni-Kanali Chris Davies anashitakiwa kwa kumbaka askari ambaye ni mama wa watoto wawili na umri wa miaka 53 katika tukio linalodaiwa kufanyika huko Kingston, Ontario, Canada.
Davies anadaiwa kumwambia mwanamke huyo kwamba: “Nina uume wenye urefu wa inchi nane (sentimita 20.3) ambao unaweza kuubomoa ulimwengu wako.” Jina na utambulisho wa mwanamke huyo vimehifadhiwa.
Mwanamme huyo anadaiwa alimfuata mwanamke huyo hadi hotelini kwake baada ya mwanamkehuyo ‘kubugia’ pombe mbalimbali za kutosha walipokuwa askari hao na wenzao wakinywa vileo.
Davies na mwanamke mwathirika walikuwa sehemu ya kundi la askari waliokuwa wakinywa vileo baada ya gwaride maalum kwenye kambi ya kijeshi ya Fort Frontenac (pichani).
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, Davies alimwuliza mwanamke huyo: “Je, tukajaribu?” Hii ni baada ya kujigamba kwamba kuhusu uume wake, jambo lililomfanya mwanamke huyo aondoke sehemu hiyo.
Mwanamke huyo aliripoti tukio hilo polisi mjini Kingston, Ontario, nchini Canada ambapo askari hao walikuwa wameungana na wale wa Canada kuadhimisha Mapigano ya Tuta (Ridge) la Vimy katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK