AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isaack Kamwelwe , ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Musoma, Gantala Said (pichani kushoto) ambaye anachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha kwenye Mradi wa Maji Bunda na akizivunja Bodi za Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira za Mikoa ya Arusha na Mara (Musoma) baada ya kujiridhisha kuwa utendaji wao siyo mzuri.
Kamwele amefikia uamuzi huo leo baada kubaini kuwa kumekuwepo na uzembe wa utekelezaji wa miradi ya serikali ya maji kwa baadhi ya watendaji katika idara hizo.
“Kufuatia ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majliwa mkoani Mara, imebainika kuwa kumekuwepo na matatizo ya huyo Mkurugenzi Gantala ambaye Waziri Mkuu ameagiza Mkurugenzi huyu watendaji wengine wachunguzwe na TAKUKURU.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK