AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na Mwananchi leo Januari 26, mwaka 2018 msemaji wa Jeshi hilo, Barnabas Mwakalukwa amesema polisi wanafanya kazi kwa kufuata kanuni, taratibu na sheria za Jeshi hilo.
Jana, Kigwangalla mbali na kutoa agizo hilo, amesema watu hao wanne pia walipanga njama za kumuua mwanaharakati, Wayne Lotter na kwamba polisi wakishindwa kuwakamata atawashtaki kwa Amiri Jeshi Mkuu ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mwakalukwa amesema jukumu lao ni kukamata wanapopata shitaka la kuwapo kwa kitu kisicho cha kawaida, kuchunguza na kupeleka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kukamilisha taratibu nyingine.
“Kazi yetu ni kukamata, kuchunguza na kupeleka kwa DPP kwa ajili ya taratibu nyingine, hatufanyi kazi kwa matamko ya bungeni,” amesema na kuongeza,
“Alichokisema mheshimiwa Kigwangalla nimekisoma kwenye vyombo vya habari akihusisha na suala la mwanaharakati aliyeuawa, sisi hatufanyi kazi kwa kufuata vyombo vya habari vimeandika nini au limetolewa tamko gani au kuna shinikizo gani, tunafanya kwa kufuata taratibu zilizopo.”
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Kwa nidhamu hawana. Wangekuwa na nidhamu wasingeshirikiana na Lugumi kuwaibia Watanzania mabilioni.
ReplyDelete