Kijana Mmoja Akamatwa na Polisi kwa Kosa la Kuiba Majeneza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kijana Mmoja Akamatwa na Polisi kwa Kosa la Kuiba Majeneza
Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Boniface mkazi wa Mwananyamala kwa Msisiri anashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa kuiba masanduku ya kuzikia (majeneza) mawili na kuyaficha nyuma ya choo cha mkazi mwengine wa mtaa huo.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, amesema tukio hilo limetokea kati ya ofisi mbili za kuuza masanduku hayo ambapo moja ndiyo iliyoibiwa majeneza hayo, ambayo moja ni la mtu mzima na moja likiwa la mtoto mdogo

“Kuna work shop mbili ambazo zinajishusisha na kutengeneza masanduku, zipo kwenye sehemu moja, asubuhi mtu kaingia kwenye work shop yake akakuta masanduku mawili hayapo akaanza kufuatilia, baada ya muda akajua yapo kwenye workshop nyingine, kwa hiyo kilichofanyika ni ufuatiliaji na askari wakafanikiwa kuyapata, ni suala ambalo linachunguzwa kujua kama wanadaiana au ni wizi umefanyika, ndipo sheria ifuate”, amesema Kamanda Muliro.

Mmiliki wa masanduku hayo Bi. Judith Carlos amesema masanduku hayo aligundua yapo kwa jirani yake baada ya kumuahidi mtu atampa elfu 50 iwapo atamsaidia kujua nani kayachukua, na ndipo baadaye akaambiwa mahali yalipo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad