AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msemaji wa umoja huo , Ebba Kalondo, amesema toni la matamshi hayo lilikera hata zaidi ikikadiriwa idadi ya Waafrika waliouzwa kama watumwa Marekani.
Umoja huo unataka rais Trump aombe msamaha.
Inadaiwa kwamba rais Trump alitoa matamshi hayo dhidi ya Africa, Haiti na Elsavador kwenye ikulu ya White house katika mkutano na wabunge wa congress.
Matamshi hayo yamekashifiwa na wengi, likiwemo shirika la kimataifa kuhusu haki za binadam.
Mwenyekiti wa tume ya muungano wa bara Afrika Moussa Faki Mahamat
Siku ya IJumaa bwana Trump alituma ijumbe wa Twitter akisema kwamba lugha aliyotumia wakati wa mkutano wake na wabunge wa Congress ili kuzungumzia swala la uhamiaji ilikuwa ngumu.
Lakini aliongezea kwamba maneno anayoshutumiwa kutoa sio lugha aliyotumia.
Botswana yamshutumu Trump kwa kutusi nchi za Afrika
Umoja wa Afrika ulisema nini?
''Matamshi yalitolewa na Trump hayana heshima ya tofauti iliopo na haki za kibinaadamu''.
Uliongezea: Huku tukionyesha kushangazwa kwetu , Umoja wa Afrika unaamini pakubwa kwamba utawala mpya wa Marekani haulielewi bara la Afrika na watu wake.
''Kuna umuhimu mkubwa wa kuwepo kwa mazungumzo kati ya utawala wa Marekani na mataifa ya Afrika''.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK