AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wazima moto karibu na mji wa New York walikimbia nyumbani kwa kiongozi huyo Clinton kukabiliana na moto uliozuka jana Jumatano jioni.
Msemaji wa familia ya Clinton ambaye hakutajwa jina lake alieleza kuwa moto huo ulizuka kwenye nyumba iliyotumiwa na maofisa wa kitengo cha ujasusi cha Secret Service.
Alisema nyumba anayoishi Bill na mkewe Hillary Clinton ambaye wakati fulani alikuwa waziri wa mambo ya nje haikuguswa na moto huo. Nyumba ya Clinton na maofisa usalama zimekaribiana.
Ripoti zinasema kuwa wakati moto huo ukizuka Rais Clinton na mkewe hawakuwepo huku msemaji huyo akifafanua kuwa "kila kitu kiko shwari." Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.
Familia ya Clinton imekuwa ikiishi katika mji wa New Castle, takribani kilomita 64 kaskazini mashariki mwa mji wa New York.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK