Mrema Kudai Mabilioni ya Hela kwa Aliyemzushia Kifo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mrema Kudai Mabilioni ya Hela kwa Aliyemzushia Kifo
Mwenyekti wa Bodi ya Parole nchini Mheshimiwa Agustino Lyatonga Mrema, amesema anaenda kufungua kesi ya madai ya mabilioni ya shilingi kwa watu waliomzushia taarifa za kifo hapo jana.


Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, Mrema amesema watu hao wamemletea tatizo kubwa sana la kushtua familia yake na watu wake wa karibu, hivyo anaelekea TCRA ili aweze kusaidiwa kuwabaini, na kuwapeleka polisi kuwafungulia kesi.

"Walivyotangaza jana Mrema amefariki kwanza nasikitika sana, kumtangazia mtu amekufa ni kweli nilihangaika jana, mke wangu alihangaika sana, watoto wangu, marafiki zangu wapenzi wangu walikuwa wanalia kwenye simu kufuatilia hizo habari kumbe ni uzushi, ni uongo habari za kijinga kabisa, nikitoka hapa sasa hivi naenda TCRA", amesema Mrema

Mrema ameendelea kwa kusema .."Nitakuwa kiongozi wa kwanza katika nchi hii kuchukua hatua kali, wanipe fidia inayostahili kwa kuniletea ujinga, nataka kujua huyu mtu aliyeanzisha huu uvumi na kuweka kwenye mitandao kwa ajili ya kunifedhehesha na kuniabisha, bilioni 20 wanilipe kwa usumbufu kwa aibu niliyopata jana".

Kwa upande mwengine Mheshimiwa Mrema amesema kitendo hiko kilimsaidia kujua ni watu gani wanampenda kweli na kina nani hawampendi, kutokana na reaction zao baada ya taarifa feki za kifo chake.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad