AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mshambulizi wa Mbao FC ya Mwanza, Habib Kiyombo amekabidhiwa kitita cha Tsh Milioni 1, Tuzo na King’amuzi kwa kuibuka Mchezaji Bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/2018. Habib amekabidhiwa zawadi hizo na Afisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude na Meneja Fedha wa Bodi ya Ligi, Ibrahim Mwayella.Habib Kiyombo akikabidhiwa kitita cha Tsh Milioni 1, Tuzo na King’amuzi cha AzamTV kwa kuibuka Mchezaji Bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/2018. Habib amekabidhiwa zawadi hizo na Afisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude na Meneja Fedha wa Bodi ya Ligi, Ibrahim Mwayella.
Habib Kiyombo (katikati)akiwa katika picha ya pamoja.
Kiyombo amekabidhiwa zawadi hizo dakika chache kabla timu yake haijaingia uwanjani kupambana na timu ya Ruvu Shootings ya mkoani Pwani na anakuwa mchezaji wa pili mzawa kushinda tuzo ya mchezaji bora baada ya Mudathir Yahya kiungo wa Singida United kushinda tuzo ya mchezaji bora katika Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara msimu wa 2017/2018 kwa mwezi Novemba, kabla ya hapo tuzo ilikuwa inachukuliwa na wachezaji
wanaotoka nje ya Tanzania.
Mwezi Agosti mshindi alikuwa ni Emmanuel Okwi wa Simba,Septemba akawa ni Shafik Batambuze wa Singida United na mwezi Oktoba akashinda Obrey
Chirwa wa Young Africans.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK