AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Simba ambayo haina kocha mkuu kwa takribani wiki tatu tangu iachane na aliyekuwa kocha wake mkuu Joseph Omog, inadaiwa ipo kwenye maongezi na kocha huyo raia wa Ufaransa mwenye historia kubwa kwenye soka la Afrika.
Velud mwenye umri wa miaka 58, anatambulika vyema kwa mafanikio aliyowahi kuyapata nchini Algeria alipotwaa ubingwa wa ligi nchini humo kwa misimu tofuati akiwa na vilabu vya ES Setif mwaka 2013, 2014 akiwa na USM Alger na Super Cup ya Algeria mwaka 2013 akiwa na USM Alger.
Tayari inadaiwa kocha huyo ambaye msimu wa 2015/16 alikuwa anaiongoza TP Mazembe yupo jijini Dar es salaam na kama maongezi yataenda vyema atatangazwa kuanza kibarua ndani ya vinara hao wa ligi kuu VPL.
Akiwa kocha wa Togo, Velud anakumbukwa kwa tukio la kupigwa risasi kwenye mkono, wakati basi la wachezaji wa timu ya taifa ya Togo liliposhambuliwa na waasi nchini Angola wakati wanakwenda kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2010.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK