AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Dishi Bovu kwa kuanza liliwachokonoa watu wa karibu wa mwanadada huyo ili waweze kuunguza picha ambapo baada ya kumpata shoga yake mmoja mzurimzuri ambaye huonekana na Tunda mara kwa mara kwenye sherehe za kiburudani (hakupenda tummulike tochi) hivi ndivyo alivyofunguka; Shoga Mtu: Aaah! Kwani Tunda hata akiwa na mbunge au waziri kuna tatizo gani? Dishi Bovu: Tunataka tu ututhibitishie, hata sisi tunajua hakuna tatizo!
Shoga Mtu: Sasa niwathibitishie vipi? Niwatumie picha wakiwa faragha?
Dishi Bovu: Kama inawezekana, tena hapo utakuwa umesafisha picha haswaa! Shoga Mtu: Haa haaa! Siwezi kufanya huo ujinga ingawa ninafahamu kwamba ni kweli Tunda yupo na mbunge, ila mtafuteni mwenyewe, si namba yake mnayo. (Twiiii…shoga huyo aliminya kitufe chekundu cha simu yake, ikakatika.)
Dishi Bovu huyoo sambamba na Tunda Baada ya Dishi Bovu kuchonga na Shoga Mtu halikupenda kuacha ‘network’ ikisachi mchelemchele, liliamua kumtafuta Tunda ili aweze kufunguka ukweli wa madai hayo.
Dishi Bovu: Tundaa… Tunda: Nambie!
Dishi Bovu: Hongera mamaa!
Tunda: Kwa lipi? Kwanza naongea na nani mwenzangu?
Dishi Bovu: Ahaaa Tundaaaa!
Dishi Bovu hapa! Tunda: Shida yako?
Dishi Bovu: Nakuona unawakimbiza wenzio mjini!
Tunda: Kina nani?
Dishi Bovu: Mastaa wenzako! Tena huyo mbunge ambaye mna-share shuka eti amekupangishia apartment Tegeta siyo?
Tunda: Simjui bhana huyo mtu unayemzungumzia. (Twiii…naye alikata simu. Ingawa alipigiwa mara kadhaa hakuweza kupokea kabisa.)
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK