AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wito huo ulitolewa jana na makamu mwenyekiti wa Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte kwenye mkutano baina yao na Serikali ulifanyika katika ukumbi wa Hazina mjini hapa na kuhudhuriwa na wabunge na baadhi ya mawaziri.
Shamte alisema katika baadhi ya maeneo, Serikali imekuwa ikifanya mambo kwa kukurupuka na kujikuta ikiwaumiza wafanyabiashara ikiwamo masuala ya kodi.
Makamu mwenyekiti huyo alisema sekta binafsi inaumizwa kwa kiasi kikubwa na uamuzi wa kukurupuka hasa wa kuwaadhibu watu wasiohusika kwa kosa la mtu mmoja.
“Wakati mwingine watu wanaumizwa sana kwa ajili ya maamuzi haya, kodi na kufunga biashara za watu ilhali kosa linakuwa la mtu mmoja. Kwa nini hamuondoi kasoro hiyo?” alihoji Shamte wazo ambalo liliungwa mkono na mkurugenzi mtendaji wake, Godfrey Simbeye.
Akijibu hoja hiyo, waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango alikiri kuwapo kwa uamuzi wa kushtukiza serikalini na kusema wakati mwingine inalazimika kufanya hivyo.
Dk Mpango alisema wakati mwingine kuna madhara kwa watu kukurupuka na kufanya vitu visivyokuwepo na kusema ndani ya Serikali, kuna baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu ambao wanafanya vitu ama kwa kukurupuka au kutokujua.
“Nakiri kweli ndani ya Serikali kuna watu ambao wanafanya mambo ya ovyo na kuisababishia Serikali hasara kubwa, lakini kuna wakati tunafanya hivyo kwa sababu inabidi tufanye hivyo kwa masilahi ya nchi,” alisema Dk Mpango.
Hata hivyo, aliwatupia lawama baadhi ya wafanyabiashara akisema wamekuwa na tabia ya kukwepa kodi jambo ambalo ni kinyume na Serikali.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK