AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza hali ya usalama ya mkoa kwa mwaka 2017 mbele ya waandishi wa habari Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga amebainisha kuwa jumla ya makosa 82,211 ya ukiukwaji wa sheria za barabarani yalipatikana katika kipindi cha mwaka 2017, wakati mwaka 2016 yalikuwa ni 66,172.
Kamanda Mpinga, alisema Mwaka jana jumla ya watu 170 walipoteza maisha kutokana na ajali za barababani wakati mwaka 2016, watu waliopoteza maisha ni 286 hivyo kuna upungufu wa asilimia 40.5 ya idadi ya vifo vilivyolipotiwa katika kipindi cha miaka miwili.
“Sababu za kutokea kwa matukio ya ajali ni kuongezeka kwa vyombo vya usafiri mkoani Mbeya hasa magari na pikipiki, baadhi ya madereva kutozingatia sheria za usalama barabarani, ikiwa ni pamoja na mwendokasi hasa usiku na ulevi licha ya jitihada za jeshi la polisi kwa kushirikiana na wadau kutoa elimu mara kwa mara” alisema.
Akizungumzia hali ya uhalifu, kamanda Mpinga alisema jumla ya makosa 26,009 yaliripotiwa kutokea katika mkoa wa Mbeya kwa kipindi cha mwaka jana ikilinganishwa na matukio 32,943 yaliyoripotiwa katika kipindi kama hicho mwaka 2016.
Aidha Kamanda Mpinga amesema kwa mwaka 2018 jeshi la polisi limeandaa mikakati mbalimbali ya kukabiliana na wahalifu na uhalifu pamoja na kupunguza ajali za barabarani ikiwa ni pamoja na kubaini muelekeo wa uhalifu na maeneo tete ili kuelekeza nguvu katika maeneo hayo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK