Jerry Muro Akoshwa na Kasi ya Okwi "Kwangu Mimi Okwi Ndiye Mchezaji Bora Chirwa Hawezi Mfikia Okwi"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jerry Muro Akoshwa na Kasi ya Okwi "Kwangu Mimi Okwi Ndiye Mchezaji Bora Chirwa Hawezi Mfikia Okwi"
Aliyewahi kuwa Afisa Habari wa klabu ya Yanga, Jerry Muro, ameeleza mtazamo wake wa kuwa nani anaweza kuwa mfungaji bora katika msimu huu wa Ligi Kuu Bara.

Muro amesema anampa nafasi kubwa mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi, kutokana na kiwango kizuri ambacho amekuwa akikionesha akiwa na Simba.

Mbali na hilo, Muro pia amemtaja mchezaji wa Yanga, Obrey Chirwa kuwa hawezi kumfikia Okwi, kwani kiwango chake si kama cha mwenzake.

Muro amesema Chirwa amekuwa akigoma kila wakati kuichezea hata timu yake, hivyo hampi na nafasi ya kuchuana na Okwi na akaenda mbali kwa kusema hastahili kulinganishwa naye.

"Kwangu mimi Okwi ndiye mchezaji bora kwa sasa, hauwezi ukamlinganisha na Chirwa ambaye amekuwa akigoma hata kuichezea Yanga, Okwi ni ''Real Proffesional" hivyo hawezi kufikiwa na Chirwa katika mbio za ufungaji bora" alisema Muro.

Okwi mpaka sasa amefikisha mabao 16 katika mechi 19 alizocheza msimu huu, wakati Chirwa ana mabao 11.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad