Ngoma, Yanga Mambo Safi Wamalizana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

SIKU chache baada ya uongozi wa klabu ya Yanga kutamka hatua yao ya kufikiria kuvunja mkataba na mshambuliaji wake, Donald Ngoma, kufuatia majeraha sugu, suala hilo sasa halipo, imeelezwa.

Ngoma, ambaye anaendelea kuuguza majeraha yake ya goti, anategemewa kuanza mazoezi wiki hii baada ya kudaiwa kupona.

Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, kwa sasa inaendelea na mazoezi yake kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini ikijiandaa na mchezo ujao wa Ligi Kuu Bara.

Mmoja wa viongozi wa timu hiyo aliliambia Nipashe jana kuwa, Ngoma anajiandaa kurejea uwanjani hivi karibuni, hivyo suala la kukatishwa mkataba wake limesitishwa.

"Hayo yalikuwa mapendekezo, kwamba kama hatorejea uwanjani kwa muda mrefu ni vyema mkataba wake ukakatishwa, lakini Ngoma ameanza kupona na hivi karibuni ataanza mazoezi mepesi kabla ya kuungana na wenzake," alisema kiongozi huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.

Kwa upande wake, Meneja wa klabu hiyo, Hafidh Saleh, alimwambia mwandishi wetu kuwa taarifa alizonazo juu ya mshambuliaji huyo ni kuwa anaendelea kupona na hivi karibuni atarejea uwanjani.

"Hayo masuala ya mkataba ni ya uongozi zaidi, mimi binafsi sifahamu, ninachojua Ngoma anaendelea kupona na mwenyewe amesema anakaribia kurejea uwanjani," alisema Saleh.

Alisema amewasiliana na mchezaji huyo na kumhakikishia kuwa taratibu ameanza kupona na anatarajia kuanza mazoezi hivi karibuni.

Wiki iliyopita, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa, alikaririwa akisema kuwa wanafikiria kuuvunja mkataba na nyota huyo kwa kuwa amekuwa na majeraha ya muda mrefu.

Katika hatua nyingine, Yanga imepanga kuelekea Shelisheli mapema zaidi kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya klabu ya St Louis ya nchini humo.

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Jumamosi iliyopita, Yanga ilifanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0.

Ili kusonga mbele, wawakilishi hao wa Tanzania Bara wanahitaji ushindi ama sare ya aina yoyote katika mechi hiyo ya marudiano.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad