Serikali Yataja Maeneo Yanayotumika Kupitisha Dawa za Kulevya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Yataja Maeneo Yanayotumika Kupitisha Dawa za Kulevya
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali imebaini maeneo ya bahari kuu, bandari, vituo vya mabasi na viwanja vya ndege ndio yanatumika zaidi kupitisha dawa za kulevya.

Amesema wafanyabiashara, wasambazaji na watumiaji wa dawa hizo wameendelea kukamatwa lengo likiwa ni kuhakikisha biashara hiyo inamalizika nchini.

Taarifa iliyotolewa leo Februari 13, 2018 na ofisi ya Waziri Mkuu imesema kuwa kiongozi huyo ametoa kauli hiyo wakati akikabidhi gari kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Sianga katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Amesema mbali na kukamata meli, pia Serikali imewakamata wasambazaji pamoja na kundi kubwa la wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara hiyo sambamba na watumiaji.

Waziri Mkuu amesema lengo ni kuhakikisha Tanzania inakuwa salama na kizazi chenye uwezo wa kuzalisha mali.

Amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika vita dhidi ya dawa za kulevya, ambapo hivi karibuni imekamata meli nyingi, moja ikiwa inatokea pwani ya Msumbiji na ilikamatiwa maeneo ya Mtwara ikiwa na dawa nyingi za kulevya.

“Ni wakati wa Serikali kuendelea kuiwezesha Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya na leo hii tunawakabidhi gari hili jipya kabisa ili iweze kuendelea na utekelezaji wa majukumu yake ipasavyo,” amesema

Pia, amewataka Watanzania waachane na biashara ya dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na kazi ya kusambaza, kuzalisha na kutumia na watakaokamatwa wakijihusisha nazo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Amesema kwa sasa Serikali inajenga maabara ambayo itatumiwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa dawa wanazozikamata.

Ameongeza kuwa wananchi wanatakiwa kushirikiana na Serikali katika vita dhidi ya dawa za kulevya kwa kutoa taarifa mara wanapowabaini wafanyabiashara, watumiaji na wasambazaji wa dawa hizo.

Pia wahakikishe wanawalinda vijana ili wasijihusishe na dawa za kulevya.

Kwa upande wake, Sianga ameishukuru Serikali kwa kuipatia mamlaka hiyo gari ambapo alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi waachane na biashara hiyo huku akiwasihi kupambana kuhakikisha dawa za kulevya haziingii nchini.

Amesema mbali na kudhibiti biashara hiyo, pia wanatoa elimu juu ya madhara ya matumizi ya dawa za kulevya vikiwemo vitendo viovu vinavyofanywa na watumiaji ili wachukie na waache kutumia dawa hizo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad