AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Uchunguzi wa gazeti hili kupitia kwa rafiki wa karibu na Tunda ulionesha kwamba baada ya video hiyo kusambaa ilikuwa ni patashika nguo kuchanika kwani wazazi wake walikasirishwa mno na kitendo hicho, ndipo wakamweka kitimoto japokuwa hadi sasa hajakaa nao sawa.
“Familia ya Tunda ilimweka kitimoto mwanadada huyo na kumsema sana ambapo aliahidi kwamba atabadilika na akawaangukia wazazi wake na kuwaomba msamaha licha ya kuwa haikuwa kazi rahisi kwa kweli,” alisema rafiki huyo.
Ijumaa Wikienda lilimtafuta Tunda ambaye alieleza kuwa, baada ya video hiyo kuvuja kulitokea mtafaruku mkubwa kwa wazazi wake huku mpenzi wake akikasirishwa na kitendo hicho na hadi sasa hazungumzi naye.
“Nimejifunza sana maana ile video imenivuruga sana kwa kweli kwani wazazi wangu walikasirika sana, mpenzi wangu mpaka sasa haongei na mimi ila bado ninaendelea kumwelewesha kwamba ile ilikuwa ni pombe tu.
“Naamini hasira zake zikiisha atanitafuta tu maana najua ananipenda, nimekoma kunywa pombe na nimeshaacha kabisa kwa kweli,” alisema Tunda.
Video hizo zilikuwa gumzo mitandaoni kabla ya Kinje kufiwa na baba yake, Mzee Kingunge hivyo watu kuacha suala hilo kwani ni kumuongezea maumivu juu ya maumivu.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK