Watu Watatu Wakamatwa na Nyara za Serikali Zenye Thamani ya Milioni 33

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watu Watatu Wakamatwa na Nyara za Serikali Zenye Thamani ya Milioni 33
Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, oparesheni na doria zenye tija ambapo February 5, 2018 katika maeneo ya Mwanjelwa Polisi wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu wakiwa na nyara za Serikali ambazo ni vipande vinne vya meno ya Tembo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya Mohammed Mpinga amewataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Kenedy Lupembe Simsokwe ambaye Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha SAUT – Tawi la Mbeya, Mathew Elikana Mwanjala ambaye ni Mpiga picha na Shaban Mkwiche.

Mpinga amesema baada ya kukamatwa na kupekuliwa, watuhumiwa walikutwa na nyara hizo ambazo ni Vipande vinne vya Meno ya Tembo ambavyo vina uzito wa Kilogram 5 na thamani yake ni Tshs 33,000,000/=. 

Kamanda Mpinga amesema taratibu za kisheria zinafanyika ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani na imeitaka jamii kuacha tabia ya kuwa na tamaa ya kujipatia utajiri wa haraka kwa kutumia njia za mkato zisizo halali, badala yake wafanye kazi halali ili kupata kipato halali.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad